Mpina apiga marufuku ‘kamatakamata’ ya mifugo
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amepiga marufuku mara moja
tabia ya baadhi ya watendaji wa Serikali katika Hifadhi za Misitu,
Mapori ya Akiba na Serikali za Mitaa, kukamata mifugo holela na kutoza
faini zisizo na misingi ya kisheria.
Aidha amesema watendaji wa serikali waliofanya hujuma na dhuluma kwa
wafugaji, hawatabaki salama, kwani serikali itawafuatilia na kuchukua
hatua stahiki kwa mujibu wa sheria.
Katika hatua nyingine, waziri huyo amesifu utendaji kazi wa Mkuu wa
Wilaya ya Handeni mkoani Tanga, Godwin Gondwe katika usimamizi wenye
weledi wa sheria za mifugo nchini.
Mpina alitoa kauli hiyo juzi akiwa wilayani Handeni, ambapo alitumia
fursa hiyo kupiga marufuku ukamataji mifugo holela huku akimtaja Gondwe
kama kielelezo cha kuwa kiongozi wa kwanza kitaifa wilayani,
anayezifahamu vizuri na kuzisimamia kikamilifu sheria za mifugo na
kuleta tija katika ukuaji wa sekta hiyo.
Alisema mbali ya kusimamia sheria, Gondwe ameweza kuanzisha kijiji
cha wafugaji, kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji na watumiaji
wengine wa ardhi na kutoa huduma bora za mifugo wakati wote.
Akizungumzia tatizo hilo la ukamataji holela wa mifugo nchini, Waziri
Mpina alisema kama sekta hiyo isingekuwa inazalisha mazao ya mifugo na
serikali kuamua kuagiza kutoka nje ya nchi, basi ingezilazimu kutumia Sh
trilioni 17.8, lakini alisema kaya milioni 4.49 nchini
zinajishughulisha na ufugaji mifugo aina mbalimbali.
“Watendaji wa serikali waliofanya hujuma na dhuluma kwa wafugaji
hawatabaki salama, tutawafuatilia na kuchukua hatua stahiki kwa mujibu
wa sheria,” alisema. Alisema Sheria ya Misitu Na. 14 ya mwaka 2002
Kifungu cha 26, inazuia mifugo kuingia kwenye hifadhi za misitu ya
kitaifa au iliyo chini ya Mamlaka za Serikali za Mitaa, ambapo pamoja na
wafugaji kuvunja sheria hiyo, bado wanahitaji kutendewa inavyostahili
kwa mujibu wa sheria za nchi ili kuweka ulinganifu wa Watanzania wote
mbele ya sheria za nchi.
Alibainisha kuwa kumekuwa na mazoea ya ukamataji holela wa mifugo,
yanayoendelea nchini ambayo yanatekelezwa bila kuzingatia Sheria ya
Ustawi wa Wanyama Na.19 ya mwaka 2008 na Kanuni zake za mwaka 2010
Kifungu cha 7 na 8 na Sheria ya Magonjwa ya Wanyama Na. 17 ya mwaka
2003.
Hivyo, alisema mifugo imekuwa ikishikiliwa kama kidhibiti kwa muda
mrefu na mingine kufa kutokana na magonjwa na ukosefu huduma ikiwemo
matibabu, chanjo na kuogeshwa ili kuepuka magonjwa ndorobo na kupe.
“Mfano mifugo iliyomatwa Pori la Akiba la Swagaswaga mwezi Septemba
hadi Desemba 13 huku ng’ombe 197 kati 411 walikufa kutokana na matatizo
ambayo yangeweza kuepukika.
“Pia katika Pori la Akiba Rukwa mifugo iliyokamatwa tangu Machi 25,
2016 ilikuwa 1,332, ng’ombe waliokufa ni 692 waliobaki ni 640 tu kufikia
Novemba 2017,” alisema. Alisema katika eneo la hifadhi ya wanyamapori,
jumla ya mifugo 2,456 walioshikiliwa kwa miezi 3, ng’ombe 151 walikufa
kufikia Novemba mwaka huu na mifugo mingine kupotea na kuuzwa bila
utaratibu, jambo alilosema ni lazima lifike mwisho.
Mpina alisema mazoea hayo, kwa upande mwingine yameonesha tofauti ya
namna wanajamii wanavyoshughulikiwa na sheria. Alitoa mfano wananchi
waliokiuka Sheria za Uhifadhi wa Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 kwa
kulima, kukata miti, kujenga na kuchunga mifugo kama shughuli za
kiuchumi, ni wale wenye mifugo tu ndio ambao mali zao hukamatwa na
kupigwa faini.
“Mazoea haya yanaendeshwa bila Wizara ya Mifugo na Uvuvi kujulishwa
ili kuchangia weledi na kupata uelewa wa pamoja ndani ya Serikali, hali
hii inaleta mkanganyiko katika utendaji wa wizara mbalimbali ndani
Serikali,” alisema Mpina.
Mpina alibainisha kuwa katika eneo la utozaji wa faini, kuna baadhi
ya maeneo ambapo operesheni za wafugaji zimekuwa zikifanyika huku
watendaji wa serikali wakidhani kuwa faini zilizoainishwa kwa mujibu wa
sheria ni ndogo, hivyo kupanga viwango wanavyoona vinakidh
Comments
Post a Comment