MBULU WAMPONGEZA KAMOGA KWA KUFANIKISHA MAENDELEO



Image result for mkurugenzi wilaya ya mbulu
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbulu Mkoani Manyara, Bwana Hudson Kamoga amewashukuru  wananchi wa Kijiji cha Masieda kwa kuonyesha ushirikiano katika  umaliziaji wa jengo la madarasa la shule ya msingi Umbur.
Afisa mtendaji wa Kijiji cha Masieda Yasenti Lazaro amezungumza wakati Kamoga akizindua madarasa matatu ya shule hiyo amesema wananchi wa eneo hilo wanashukuru kwa kuwezesha umaliziaji wa jengo la madarasa la shule hiyo.
Bwana Lazaro amesema shule hiyo imeanzishwa mwaka 2014 na kusajiliwa mwaka 2015 ina wanafunzi 335 na vyumba vinne vya madarasa.
Mwenyekiti wa Kata ya Masieda, Nicomed Nada ameshukuru Rais John Magufuli kumteua Kamoga kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kwani anawatumikia wananchi kwa kuacha alama ya maendeleo.
Bwana Kamoga amesema baada ya kuzungumza na wadau wa maendeleo, wakawezesha fedha hizo na kufanikisha ujenzi huo wa madarasa, ambapo shilingi milioni  (7) zimemalizia ujenzi huo na shilingi milioni  3 zikatumika kwenye utafiti wa maji katika Kijiji cha Mamagi na Genda.

Comments

Popular posts from this blog

Nyota ya Simon Msuva yazidi kungáa katika klabu yake ya Difaa El Jadid

MFANYAKAZI WA PPF AKAMATWA AKISAFIRISHA MIRUNGI

SAKATA LA AIRTEL LAZIDI KUKOLEA....TEWUTA NAO WAIBUKA