MAVUNDE AWATAKA POLISI JAMII KUUNDA VIKUNDI VYA UZALISHAJI MALI KUJIKWAMUA KIUCHUMI
Naibu Waziri wa Nchi-Ofisi ya Waziri Mkuu( Kazi,Vijana na Ajira) Anthony Mavunde amewataka Vijana ambao wanashiriki katika mafunzo ya Ulinzi shirikishi kupitia Polisi Jamii kuunda vikundi vya uzalishaji mali ili kujikwamua kiuchumi na kuongeza kipato.
Mavunde
ameyasema hayo leo wakati akifunga mafunzo ya Ulinzi shirikishi
yaliyoshirikisha Vijana 75 katika kata ya Mtumba,Manispaa ya Dodoma.
“Pamoja
na jukumu kubwa mlilonalo na ulinzi na usalama wa raia na mali
zao,lakini pia mhakikishe mnatumia mkusanyiko wenu kuunda vikundi vya
uzalishaji mali ili kujiongezea kipato na kutengeneza nafasi za Ajira
zaidi,”amesema
Mavunde
amewataka vijana hao kuyatumia vyema mafunzo waliyopata kwa kuwa
waadlifu,waaminifu na wazalendo kwa Taifa lao na kusimama mstari wa
mbele kuhakikisha Taifa hili linaendelea kuwa na AMANI na UTULIVU.
Naye,
Kamanda wa Mkoa wa Polisi wa Dodoma,SACP Gilles Muroto amewataka
Vijana zaidi kujitokeza katika Ulinzi shirikishi ili kuimarisha usalama
na amani katika mkoa wa Dodoma.
Comments
Post a Comment