Kampuni
ya SGA Security imeadhimisha miaka 33 tangu ianze shughuli zake nchini
Tanzania huku ikiwatunuku wafanyakazi walioitumikia kampuni hiyo kwa
muda mrefu na kupongezwa na Jeshi la Polisi kwa hatua hii.
Shughuli
ya kuwatambua wafanyakazi hawa ilihudhuriwa na Kamanda wa Polisi Mkoa
wa Kipolisi wa Kinondoni, SACP Jumanne Muliro katika ofisi za SGA Masaki
ikiwa ni moja ya majukumu yake kuhakikisha makampuni binafsi ya ulinzi
na usalama yanaendeshwa kwa viwango vinavyotakiwa.
Kampuni
hiyi iliunda kikundi maalumu kijulikanacho kama ‘Club 20’ ambacho
kinajumuisha wafanyakazi walioitumikia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka
20.
Kwa
sasa kampuni ya SGA Security imeajiri wafanyakazi zaidi ya 5,100
Tanzania na kuifanya iwe moja ya makampuni makubwa ya usalama nchini.
SACP
Muliro aliipongeza SGA kwa kujali masilahi ya wafanyakazi na kuongoza
kwa mfano huku akisisitiza kuwa makampuni mengi ya ulinzi na usalama
hayafuati utaratibu uliowekwa ikiwemo mafunzo, usimamizi na mishahara
huku akitoa wito kwa makampuni mengine kuiga mfano wa SGA.
Comments
Post a Comment